
Mtemvu, aliongeza kwamba yeye kwa kushirikiana na madiwani wameandaa mkakati wa kuchangisha pesa ili shule zote ziwe na madawati ya kutosha
Afisa elimu wa msingi wa Manispaaya Temeke, Honorina Mumba, alimshukuru Mbunge huyo kwa kujikita katika elimu kwa kuhakikisha matatizo mbalimbali yanapatiwa ufumbuzi.
Alisema madawati hayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuziba pengo lilopo la ukosefu wa madawati kwa shule za msingi na wanatarajia kwa nguvu zake pamoja na madiwani suala hilo litafikia mwisho.
NA MOSHI LUSONZO, NIPASHE
No comments:
Post a Comment
Tuandikie maoni yako kuhusu habari hii
Asante kwa Mchango wako