Friday, 7 February 2014

Mbunge Msigwa afikishwa kortini akidaiwa kujeruhi

MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumjeruhi kada wa Chama Cha Mapunduzi (CCM) kwa kitu kitu kizito. Mchungaji Msigwa  alifikishwa  katika mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, Godfrey Isaya jana na kusomewa shitaka moja la kujeruhi. Akisoma shitaka hilo Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Elizabeth Swai alidai Mchungaji Msigwa alitenda kosa hilo Febrauri 5, 2014 katika kijiji cha Nduli  mjini Iringa. 
Alidai  Mchungaji Msigwa anashitakiwa kwa kumjeruhi Salum Kahita.


Mchungaji Msigwa anayetetewa na wakili Lwezaula Kaijage alikana kosa hilo na hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 18  mwaka huu. Mbunge huyo yupo nje kwa dhamana.  

Jeshi la Polisi pia limewapandisha kizimbani Meshack Chonanga (22) na Paulo Mapunda wote wakazi wa Kijiji cha Nduli mjini Iringa kwa madai ya kumjeruhi Alex Mpiluka  ambaye ni mwanachama wa Chadema wakati wa kampeni hizo.

Kukamatwa kwa mbunge huyo kulitokana na vurugu   kubwa  zilizoibuka juzi katika kampeni za uchaguzi mdogo  wa udiwani Kata ya  Nduli, Manispaa ya Iringa.

Katika kampeni hizo inadaiwa wafuasi wa Chadema waliwashambuliwa  wafuasi wa CCM  kwa mawe na nondo ambako kijana mmoja,   Salum Kaita  alijeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa kwa matibabu.

Mashududa wa tukio hilo walisema kuwa wakati vijana wa CCM wakiwa katika mkutano wa kampeni ghafla walivamiwa na wafuasi wa Chadema waliowashambulia kwa mawe na nondo.


NA RAYMOND MINJA, IRINGA

No comments:

Post a Comment

Tuandikie maoni yako kuhusu habari hii
Asante kwa Mchango wako