Tuesday, 4 February 2014

Njombe: Kada wa CHADEMA avunjwa taya, watatu wawekwa ndani

INASIKITISHA LAKINI IMETOKEA

Katika hali isiyotarajiwa kamanda mmoja wa chadema mkoani njombe amevunjwa taya leo hii katika eneo la matalawe kwenye jimbo la Mama ANNA MAKINDA.

Haya yametokea baada ya kamanda huyo ambaye ni kiongozi wa ulinzi kanda ya nyanda za juu kusini bwana KALONGA kuwafumania viongozi wa chama cha MAPINDUZI wakigawa fedha kwa wananchi ili wawapatie vitambulisho vyao vya kupigia kura.

Kalonga na viongozi wengine walizingirwa na viongozi wa chama mapinduzi na kuanza kupokea kipigo kitakatifu ambacho kilipelekea taya zake kuvunjika vibaya.

polisi walipofika waliwakamata na kuwapeleka kituoni ambapo viongozi watatu wamewekwa ndani huku aliyeumizwa akakicheleweshwa kwa makusudi kupelekwa hospitali huku wakitoa kauli zilizokosa ubinadamu.

Anayeratibu zoezi hili kwa karibu kabisa ni mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa na mbunge wa jimbo la njombe kaskazini bwana ja people ambaye mudda wote yupo karibu a polisi ili kuhakikisha wanaihujumu chadema

Nitaendelea kuwapa taarifa kwa kadiri ninavyoweza ila kwa sasa narudi polisi kupigania kamanda wetu atoke ili akatibiwe

MUNGU ISIMAMIE CHADEMA

MUNGU ITAZAME TENA TANZANIA


No comments:

Post a Comment

Tuandikie maoni yako kuhusu habari hii
Asante kwa Mchango wako