Friday, 31 January 2014
Malecela amvaa Edward Lowassa
- Ni mbio za urais 2015
- Amtuhumu kumwaga fedha

Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samuel Malecela, akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) moja ya fulana iliyoandikwa Friends of Edward Lowassa (Marafiki wa Lowassa)
Tuesday, 28 January 2014
Hivi kwa nini wabunge wa CHADEMA wanakuwa waongo waongo?

Wakuu,mimi huwa nakereka sana ninapohudhuria mikutano ya baadhi ya wabunge wa CHADEMA.
Nianze hivi,
Ukienda jijini mbeya karibu eneo kubwa la barabara za mitaa zimepigwa lami,sasa BWANA JOSEPH MBILINYI anajitapa kuwa yeye ndo aliyeleta hiyo lami kana kwamba alitoa pesa yake mfukoni. Jamani,hizi barabara ni mpango wa uboreshaji wa majiji na bado ilikuwa ni utekelezaji wa ilani ya chama kilichopo madarakani.
Hatimaye Mh, January Makamba atimiza umri wa kugombea Urais

Leo 28/January 2014, kijana na mwanasiasa machachari na mwenye maono makubwa ya kiongozi ndugu January Makamba ametimiza miaka 40 ambao ni umri unaotakiwa kikatiba kugombea urais
Mbowe apaisha homa serikali 3

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema iwapo kutakuwa na uchakachuaji wa rasimu ya Katiba mpya na kuondoa mapendekezo ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya mfumo wa serikali tatu, chama hicho hakitakubali na hatua madhubuti zitachukuliwa. Mbowe aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Biharamulo mkoani Kagera na Chato, mkoani Geita.
- Sugu atamba maofisa wake hutoa siri kwao
- Asema ni kutokana na Serikali kutokuwa makini
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema mafanikio kinayopata yanatokana na maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa kutoa siri kwao. Kauli hiyo imetolewa juzi mjini hapa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu), wakati akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya Ruanda, Nzovwe.Alisema hatua ya nchi kuyumba, inatokana na Serikali kutowajali maofisa wa Idara hiyo, hali inayowalazimu kuvujisha siri kwao.
Mbunge awezesha vikundi vya wanawake

Mbunge wa viti Maalum (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro, Betty Machangu, amewashauri wananchi na vikundi vya ujasiria mali vya kinamama na vijana mkoani humo kuhakikisha wanajiunga katika vikundi ili iwe rahisi kupata misaada ya kuinua vipato vyao kutoka serikalini na baadhi ya taasisi mbalimbali nchini. Machangu aliyasema hayo juzi mkoani Kilimanjaro katika ziara yake ya kuhamasisha vikundi vya wajasiriamali na kutembelea vikundi vyote vilivyopo katika Wilaya ya Moshi Vijijini na kuvipatia fedha baadhi ya vikundi.
Monday, 27 January 2014
Vicent Nyerere:Ukimtumia polisi sms ya tafadhali nipigie,atakujibu kwa sms ya niongezee salio!

Akiongea muda huu katika kipindi cha ITV cha "dakika 45" waziri kivuli wa mambo ya ndani,mh.Vicent Nyerere (pichani) ametoa kali kwa kusema kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili polisi wetu leo hii ukamtumia polisi ujumbe wa "tafadhali nipigie",yeye atakujibu kwa ujumbe wa "tafadhali niongezee salio"!
Tuhuma Baraza la Mawaziri
- Lipumba atilia shaka elimu ya waziri wa fedha
- Yeye amjibu kwa kutoa vielelezo lukuki

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amelishushia tuhuma nzito Baraza la Mawaziri, baada ya kudai baadhi ya mawaziri walioteuliwa hawana elimu ya kutosha. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Profesa Lipumba alisema mmoja wa mawaziri hao ni Waziri wa Fedha, Saada Mkuya.Alisema chama chake, kina wasiwasi na elimu ya Waziri Mkuya, kutokana na wasifu wake kutoonyesha vyuo alivyosoma wakati wa kupata shahada ya kwanza na ya pili katika masuala ya biashara.
CHADEMA hamuwezi kutwaa dola kwa Chopa na Maandamano, waelezeni wananchi mtawafanyia nini

Wanaukumbi.
Chama chochote makini lengo lake ni kutwaa dola, kutwaa dola kuna kuja baada kuwaeleza wananchi nini dhumuni lenu kama chama cha siasa, wananchi wanataka kufahamu mtawafanyia nini kama wakiwachagua kuingia Ikulu, kwenye masuala muhimu Afya, Elimu, Kilimo, Uchumi wa Nchi, Mahusiano ya Kimataifa, Ajira kwa Vijana, tatizo la watanzania siyo Chopa wala maandamano.
VYAMA VYA SIASA VINAPIGA TEKE MASLAHI YA UMMA!
Hakika kujikwaa ni jambo la bahati mbaya kwa mtembezi aliye makini na ni jambo la kawaida kwa mtembezi asiye makini! Na ni mtembezi makini pekee ambaye atathubutu kujiuliza pale atakakapokuwa amejikwaa, yule asiyekuwa makini hatojiuliza kamwe.Tangu kuingia kwa muhula wa pili wa Serikali ya awamu ya nne, Watanzania wameshuhudia matukio ya kushtusha mno ndani ya vyama vya siasa.Vyama vya siasa vimekuwa vikitoa maamuzi ambayo yamekuwa yakivuruga maslahi ya wananchi wapiga na kuacha sononeko kwa umma.
Mbowe: Niko tayari kwenda jela kwa kudai katiba mpya

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeendelea na ziara zake za Operesheni Movement For Change (M4C) na ‘Pamoja Daima katika maeneo kadhaa nchini huku viongozi wake wakuu wakizungumzia mambo makuu yanayoikabili nchi. Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, akiwa mkoani Kagera, alisema yuko tayari kuwa wa kwanza kufungwa kwa kosa la kudai katiba mpya itumike ikiwa serikali italazimisha kuendelea kutumia katiba ya zamani.
Friday, 24 January 2014
CCM yamgeukia Balozi Sefue
- Yadai kauli yake kwa mawaziri mizigo ina ukakasi

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimempinga Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, kutokana na hatua ya kuwatetea baadhi ya mawaziri mizigo waliorudishwa tena kwenye Baraza la Mawaziri, huku kikisema kauli yake ina ukakasi. Msimamo wa CCM umekuja siku chache, baada ya Balozi Sefue kutangaza mabadiliko ya Baraza la Mawaziri na kuwatetea mawaziri mizigo kwa kile alichosema hawapaswi kulaumiwa kutokana na wakati mwingine kucheleweshewa fedha kwenye wizara zao.
CHADEMA,Zitto ,Mbowe na 48 LAWS OF POWER

Hapa JF tuliwahi kumjadili Kikwete zamani kwa kutumia kitabu hiki maarufu '48 laws of power'
http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la...r-2-print.html, leo ningependa tukitumie kitabu hiki kujadili yaliyotokeaCHADEMA hasa kwa Zitto na Mbowe na viongozi wote kwa kutumia kitabu hiki.....
- Je ni sheria zipi Zitto alizitumia vizuri au alishindwa kuzitumia?
- Mbowe aliweza zipi? zipi alishindwa na wengineo mfano kina Lissu na Mnyika na Lema wana tumia zipi na zipi wanashindwa...
................naamini itakuwa kitu cha kujifunza kwa kila mtu................
Na The Boss, JF
Mikutano ya M4C - Operesheni Pamoja Daima, Kigoma, Mbeya, Rukwa, Manyara na Arusha

Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe akiongoza maaandamano Kuelekea Himo kwenye Uzinduzi wa Operesheni Pamoja Daima
Mamilioni ya Lowassa yaingia CHADEMA?
Katika kile kinachoonekana kujihakikishia Urais 2015 aliyewahi kuwa waziri mkuu (sio waziri mkuu mstaafu kwani uwaziri sio nafasi ya kuajiriwa na kisha kustaafu) ndugu Lowasa ameanza ama anaendeleza kazi ya kuwamgia mamilioni viongoz wakuu wa chadema katika kumsafishia njia. Najua suala hili litashtusha wengi lakini ndio uhalisia kwani tangia mwaka 2010 viongozi wa kitaifa wa CHADEMA wamebakia kuwaandama viongozi wengine wa CCM huku wakifumbia madudu na uchafu anaoendelea kuufanya Lowasa kama kwamba hawaoni hadi hatua ya wanachama na wapenzi kuanza kuhoji kwa nn Lowasa hazungumziwi? ambapo majibu rahisi na yasiyo na mshiko kutoka kwa viongozi wa chama ni kwamba Lowasa kwa kuwa atapishwa na CCM mwaka 2015 kugombea urais sio sawa kumzungumzia kwa sasa kwani kutampa mwanya wa kujisafisha katika kashfa zake na hivo kukosa hoja za kumchafua kwa wananchi kama ilivyo kawaida ya siasa za Tanzania ili upendwe unatengeza fitina mwenzio achukiwe. ukweli ni kwamba Lowasa amekuwa akiwapa mamilioni viongozi hao ili kuwadhoofisha wapinzani wake na hatimaye kujihakikishia kupitishwa na chama chake kugombea uraisi.
Zitto ruksa kukata rufaa Chadema

Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) umempelekea Zitto Kabwe taarifa ya kikao cha Kamati Kuu kilichomvua madaraka yake ndani ya chama hicho ili aweze kukata rufaa. Habari za kutoka ndani ya Chadema zinaeleza kuwa Kamati Kuu ya chama hicho ilifikia uamuzi huo wakati wa vikao vyake vilivyofanyika kati ya Januari 3 na 4, mwaka huu. Kutokana na uamuzi huo, Zitto sasa ataweza kukata rufaa ya kupinga kuvuliwa madaraka kwenye Baraza Kuu la chama hicho.
Uteuzi wa Kikwete waikoroga CCM

Uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete kuwaacha katika Baraza la Mawaziri, mawaziri wote waliotajwa na CCM kuwa wameshindwa kutekeleza majukumu yao umekichanganya chama hicho, baada ya jana kusema kuwa hakitasita kuchukua hatua kali dhidi ya mawaziri hao na wengine, iwapo watashindwa kurekebisha upungufu wa kiutendaji unaozikabili wizara zao.
Balozi Ali Abeid Karume: “Tunataka Serikali mbili, kuujenga Muungano wetu”.

BALOZI Ali Abeid Aman Karume (pichani) ambaye pia ni MNEC wa Chama cha Mapinduzi CCM, Amesema Taifa linaitaji muundo wa Serikali mbili ilikuujenga Muungano thabitio uliasisiwa na viongozi wakuu ambao wameufikisha hapa ilipo sasa. Balozi Ali Karume alisema hayo jioni ya leo (Januarin23) kwenye mkutano wa hadhara wa kumnadi Mgombea wa nafasi ya Uwakilishi kwa chama hicho kupitia jimbo la Kiembesamaki, Mahmoud Thabit Kombo, ambapo aliwataka wanakiembe samaki kumchagua mgombea huyo ilikwenda kuwatetea na kuwatumikia katika kuunda mambo mbalimbali ikiwemo suala hilo la Muungano na Serikali mbili.
Chadema yawasilisha pingamizi dhidi ya Zitto
.jpg)
Mawakili wa chama CHADEMA, Tundu Lissu (kushoto) na Peter Kibatala
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimewasilisha majibu na pingamizi la awali dhidi ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kuhusu Kamati Kuu ya Chama hicho akiitaka mahakama kuzuia uanachama wake usijadiliwe hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa. Kadhalika, chama hicho kimejibu barua ya Zitto pamoja na kuwasilisha mwenendo wa shauri lililopelekea kuvuliwa nyadhifa za uongozi katika chama hicho kama mlalamikaji alivyoomba.
Thursday, 23 January 2014
Chadema yawaonya wabunge CCM

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema kuwa chama hicho kitachukua uamuzi mgumu ikiwa wabunge wa CCM watajikita katika kulinda masilahi yao kwenye Bunge Maalumu la Katiba kinyume na maoni ya wananchi. Alisema hayo jana katika Wilaya ya Nyasa na Mbinga kwenye siku ya kwanza ya Operesheni Pamoja Daima. Katika operesheni hiyo, ambapo aliruka kwa helikopta katika sehemu mbalimbali, alihutubia mikutano katika maeneo ya Mbamba Bay, Mbinga, Peramiho, Namtumbo na Songea Mjini.
JK kufyeka 2,500 Bunge la Katiba
- Ni asilimia 7.4 tu watakaopenya
- Majina hadharani mapema wiki ijayo

Majina ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete sasa yatawekwa hadharani wiki ijayo. Hata hivyo, Rais Jakaya Kikwete atakuwa na mtihani mgumu wa kuteua majina ya wajumbe hao kutoka asasi mbalimbali kutokana na idadi kubwa ya majina yaliyowasilishwa Ikulu na asasi hizo kulingana na nafasi ndogo za kuteua. Jumapili iliyopita, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema kuwa majina ya watu 2,722 yaliyowasilishwa kwa Rais kutoka makundi hayo yalikuwa yanaendelea kuchambuliwa.
Ufafanuzi wa CCM kwa umma kuhusu “Mawaziri mizigo”

Mara baada ya kuundwa kwa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa inayoongozwa na Katibu Mkuu Ndg. Abdulrahman Kinana mwanzoni mwaka mwaka jana, Sekretarieti hiyo imejiwekea utaratibu wa kufanya ziara mikoani kukutana na wananchi kusikiliza kero zao,kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuimarisha Chama mikoani. Utaratibu huu ni agizo la mkutano mkuu wa Taifa wa nane wa CCM uliofanyika Novemba 2012 mjini Dodoma. Nanukuu azimio hilo;
Wednesday, 22 January 2014
Ratiba ya M4C- Operesheni Pamoja Daima, Ruvuma, Tabora na Tanga
Kama ambavyo jana umma wa Watanzania ulitaarifiwa kupitia kwenye mkutano wa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe na wanahabari, Chama leo kinaanza operesheni ya takriban wiki mbili kwa nchi nzima (mijini na vijijini). Kuna jumla ya timu 6 zilizoko uwanja wa mapambano kuendesha M4C- Operesheni Pamoja Daima, ambazo zote zinaanza kazi leo katika maeneo zilizopangiwa. Timu tatu zitakuwa zikishambulia kutokea angani na timu tatu zitakuwa zikisonga mbele nchi kavu.
Prf,Lipumba:Kiembe samaki mchagueni mgombea wa CUF ayaendeleze aliyoyaacha Mansour

Mgombea wa nafasi ya uwakilishi jimbo la kiembe samaki Bwana Abdull Malik Haji akiwa pamoja na Mwenyekiti wa Chama Taif Prf.Lipumba baada ya kukabidhiwa manufesto ya chama.[/captio0n]Chama cha Wananchi CUF kimesema hakiutokuwa tayari kudhulumiwa na kufanyiwa hujuma kama zilizofanywa katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Bububu.
Raza awang’akia wanaotaka atimuliwe uanachama CCM

Zanzibar. Mwakilishi wa Jimbo la Uzini (CCM), Mohamed Raza Dharamsi amesema hakuna kifungu wala mwongozo wowote wa CCM unaomzuia mwanachama kutotumia demokrasia ya kukosoa ikiwemo muundo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Raza alitoa msimamo katika majibu yake ya maandishi alipotakiwa kujieleza mbele ya kamati ya siasa ya jimbo na wilaya huko Uzini Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja hivi karibuni.
Mbunge wa Chalinze , Said Bwanamdogo , CCM , afariki dunia

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne S. Makinda (Mb), anasikitika kutoa taarifa ya kifo cha Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe. Saidi Ramadhani Bwanamdogo Kilichotokea leo (Jumatano) asubuhi tarehe 22.1.2014 Katika hospitali ya Muhimbili/MOI alikokuwa amelazwa kwa Matibabu.
Mipango ya Mazishi zinaendela kufanywa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya Marehemu, ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho siku ya Alhamisi tarehe 23 Januari, 2014 kijijini kwake MIONO, Wilaya ya BAGAMOYO, Mkoa wa PWANI. Taarifa zaidi juu ya msiba huu zitaendelea kutolewa na Ofisis ya Bunge kadrizitakapopatikana.
“Inna llilah Waina Illaih Rajiun!”
Imetolewa na
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusianao wa Kimataifa,
Ofisi ya Bunge,
DAR ES SALAAM
22.01.2014.
RASIMU YA KATIBA KUCHAPWA GAZETI LA SERIKALI IJUMAA HII
Kifungu 20 (2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura 83, Toleo la 2013 inamtaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchapisha kwenye Gazeti la Serikali Rasimu ya Katiba ndani ya siku thelathini (30) baada ya kukabidhiwa rasimu hiyo na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue inaeleza kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, alikabidhiwa Rasimu ya Katiba tarehe 30 Desemba, 2013, na ataichapisha kwenye Gazeti la Serikali litakalotolewa Ijumaa, tarehe 24 Januari 2014.
Mnyika amvaa Magufuli

Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika amemtaka Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli na Wakala wa Barabara (Tanroads) waelekeze nguvu katika kusimamia ujenzi wa mradi wa mabasi yaendayo kwa haraka (BRT) kutoka Ubungo hadi Chalinze. Amemtaka Waziri Magufuli pia kuipitia, kuiheshimu na kuwezesha utekelezaji wa maamuzi ya mahakama juu ya hukumu ya kesi ya wananchi wa maeneo hayo ambao wanapinga kuondolewa kupisha ujenzi wa barabara hiyo.
Chadema kutikisa nchi; Helikopta tatu kurushwa nchi nzima

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuanzia leo, kinarusha helkopta tatu kwa siku 14 mfululizo, katika kutekeleza kampeni iliyopewa jina la Operesheni Pamoja Daima (ODB) itakayoendeshwa katika mikoa yote nchini. Ziara hiyo inaanzia katika mikoa ya Tanga, Mwanza na Ruvuma, huku viongozi wa chama hicho wakijigawa katika makundi sita; matatu yakitumia helkopta na matatu yatawafikia wananchi kwa kutumia usafiri wa magari.
Monday, 20 January 2014
Sikurudisha fomu kwa kuwa CHADEMA imepoteza mwelekeo
Aliyetarajiwa kuwa mgombea wa udiwani wa Kata ya Mtae wilayani Lushoto kupitia CHADEMA na kutojitokeza kurejesha fomu hatimaye amejisalimisha polisi. Mgombea huyo, Ali Said Jaha alijisalimisha juzi Jumamosi asubuhi katika Kituo cha Polisi cha Lushoto na kutoa maelezo kwamba hakuwa amepotea kama ilivyokuwa imeenezwa kwenye mitandao ya kijamii.Alisema wakati wa kurejesha fomu siku ya Alhamisi Januari 16 mwaka huu kulikuwa na matatizo ya kifamilia nyumbani kwake hivyo ikamlazimu kuyapa kipaumbele hatimaye akajikuta akiwa amechelewa kuwasili ofisi za Kata ya Mtae.
Hali bado tete CHADEMA
- CHADEMA HALI BADO TETE.
- SASA NI MBOWE vs SLAA.

Baada ya kutokufanikiwa kumvua uanachama wake na kufanikiwa kumvua nyadhifa zake zote ndani ya chama na ndani ya bunge sasa hali sio nzuri ndani ya chama na hasa viongozi wakuu M/kiti na Katibu wake ndani ya chama. Mwanaripota wetu ndani ya mtaa wa UFIPA yaliopo makao makuu ya chama anadai kumekuwepo na vikao vya Mara kwa Mara baada tu kusigana na Mzalendo zito zuberi kabwe.
Mbatia ashinda tena NCCR, mizengwe yatawala mkutano

Uchaguzi Mkuu wa nane wa Chama cha NCCR-Mageuzi, umemchagua tena James Mbatia kuwa mwenyekiti wa chama hicho kwa kipindi kingine cha miaka mitano ijayo huku mizengwe ikitawala katika uchaguzi huo. Katika uchaguzi huo ulioanza juzi, idadi kubwa ya wajumbe walikuwa na mkakati wa kumng’oa Katibu Mkuu, Samwel Ruhuza aliyekuwa akitetea nafasi yake, Mosena Nyambabe na Rehema Sam waliokuwa wakiitaka nafasi hiyo.
Dr. Slaa: Baraza jipya limechoka kabla halijaanza kazi

Katibu mkuu wa Chadema Dr. Willbrod Slaa amesema kwamba baraza jipya la mawaziri lililoteuliwa na kutangazwa jana na katibu mkuu kiongozi limechoka kabla halijaanza kufanya kazi. Aidha Dr. Slaa amesema kuwa uteuzi wa Mwigulu Nchemba kama naibu waziri wa fedha (sera) ni mkakati wa CCM kujichotea fedha za uchaguzi mkuu ujao hivyo tutarajie EPA nyingine.
Mambo matatu yaitesa CCM
MBIO za kusaka urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), na uteuzi wa nafasi nne za mawaziri, vinaelezwa kukibomoa chama hicho, Tanzania Daima limedokezwa. Mbali na mambo hayo, mchakato wa uundwaji wa katiba mpya ambayo rasimu ya pili imetoka hivi karibuni na kuingizwa kwa serikali tatu, umeonekana kukiathiri zaidi chama hicho kinachotaka uwepo wa serikali mbili. Tayari viongozi wa CCM wameshaanza maandalizi ya kukutana na wabunge, wawakilishi na wabunge wa Bunge la Katiba watakaochaguliwa, kwa lengo la kuweka msimamo wa kutopitisha serikali tatu wakati wa majadiliano.
MHE EZEKIEL MAIGE - UFAFANUZI WANGU KUHUSU TUHUMA KUWA NINAMILIKI NYUMBA YA KIFAHARI

Wapendwa,
Salaam za pilika za maisha?
Nimeona ni vema nikawafafanulia, kwa baadhi ambao hamkufuatilia kipindi cha Medani za Siasa kilichorushwa na Star TV jana mchana.
Nimeona nifanye hivyo baada ya upotoshaji wa kitoto, uliojaa roho mbaya na chuki za makusudi uliofanywa na mtu anayejiita Kiroba kwenye mtandao wa Jamii forums.
Star TV hufaya kipindi cha Medani za Siasa kwa wanasiasa mbalimbali kila wakati. Katika vipindi vyao, huongea na mwanasiasa wanayemchagua kwa wakati huo na humuuliza mambo mengi yanayomuhusu na mambo yake ya siasa.
Chuki zaanza ndani ya CCM, Sinyanga, Monduli, Mgeja, Lowasa

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja akizungumza na wanachama. Picha na Mwandishi Wetu
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja ameonya baadhi ya viongozi wa chama hicho kuwajengea chuki wanachama kadhaa na viongozi kwa madai wako karibu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa. Hatua ya Mgeja imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku ‘Msukuma’ kumkana na kumshutumu, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM, Mgana Msindai kuwa anawalazimisha kuwa nyuma ya Lowassa wakati sivyo ilivyo.
Sunday, 19 January 2014
Taarifa ya Mbunge, Cyril Chami kuhusu ukurasa ulioanzishwa kwa jina lake Facebook

Naitwa Cyril August Chami (PhD) Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini na Mjumbe wa NEC-CCM kupitia Wilaya ya Moshi Vijijini.
Nimesikitishwa na kufadhaishwa sana na mtu au watu waliotengeneza akaunti kwa jina langu kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook na kujifanya yeye au wao ndio mimi.
Wamepachika hata picha zangu zinazopatikana kirahisi kwa sababu ya majukumu ambayo nimeshawahi kuwa nayo kama Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, na Waziri wa
Viwanda na Biashara.
Vurugu CHADEMA zitaua imani ya wananchi; Mbowe, jenga chama ndani ya umma

Mbowe: Jenga chama ndani ya umma, acha mahakama
JE, kuna haja ya mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe kumburuza Zitto Kabwe mahakamani kwa madai ya kumtuhumu kupokea fedha kutoka kokote kule?
Ushauri: Hakuna haja wala sababu.
Vyombo vya habari vimeripoti wiki hii kuwa Mbowe “anasadikiwa” kuwa na nia ya kumshitaki Zitto Kabwe mahakamani.
Kisa? Eti Zitto, ambaye tayari amenyang’anywa unaibu katibu mkuu wa chama na unaibu msemaji mkuu wa upinzani bungeni, “amemdhalilisha” Mbowe kwa kumtuhumu kuchukua fedha kutoka kwa Nimrod Mkono na Rostam Aziz.
Sabodo: CCM itaanguka

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Mustapha Sabodo (pichani), amevitaka vyama vya upinzani nchini kuungana ili kuking’oa Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani. Amesema iwapo Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi vitaunganisha nguvu pamoja kwa kumsimamisha mgombea urais mmoja katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, kazi ya kuing’oa CCM madarakani itakuwa rahisi.
Hivi CHADEMA mmeshawahi kusema mtawafanyia nini watanzania?
Kila siku katika mikutano yenu ni kulaani mabaya yanayofanywa na baadhi ya watendaji ndani ya chama tawala, e.g Mara oo Wauza madawa ya kulevya, mara meno ya tembo, fulani sijui fisadi! Tena bila ushahidi! Na katika mikutano yenu ni hayo tu! Lakini hakuna hata mkutano mmoja ambao mmeshawahi kueleza mkitawala mtafanya nini kwa kumuendeleza mtanzania. Mna mkakati gani wa kutawala na mmejipanga vipi zaidi ya kubwabwaja mambo ya ufisadi!?
Na R, JF
Mbowe aitahadharisha CCM kuhusu Serikali Tatu

Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia akizungumza kwenye mkutano mkuu wa chama hicho jana. Picha Michael Jamson
Leticia Ghati na Haji Ambar Khamis jana wamechaguliwa kuwa Makamu Wenyeviti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, katika Mkutano Mkuu wa Nane wa chama hicho uliofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee. Ghati ambaye amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti (Bara) alikuwa akiwania nafasi hiyo na Anyimike Mwasakalali, Rakia Abubakar Hassan na Danda Juju ambao walijitoa kugombea dakika za mwisho.
Dk. Slaa awapuuza ATC-Tanzania

KATIBU wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa, amepuuza majigambo ya Chama kipya cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania), kuwa kitakisambaratisha chama hicho kutokana na kuchukua wafuasi wengi. Akizungumza na MTANZANIA Jumapili juzi, Dk. Slaa, alikishangaa chama hicho na kusema kuwa hayo ni maoni yao, hivyo hawezi kuongea chochote na kwamba anawashangaa kwa kujiona wako sahihi kusema hivyo.
BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
______________________________ ________________
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-
1.0 OFISI YA RAIS
Hakuna mabadiliko.
2.0 OFISI YA MAKAMU WA RAIS
2.1 Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko
2.2 Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb) Waziri wa Nchi (Mazingira).
2.3 Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb) Naibu Waziri
3.0 OFISI YA WAZIRI MKUU
Hakuna mabadiliko
MADENI ANAYODAIWA FREEMAN MBOWE NA CHADEMA

MADENI YA UCHAGUZI
"Kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mhe. MBOWE alitufahamisha wanachama kuwa alikuwa anakidai chama US $ 181,949.00 sawa na Tshs. 218,338,546. Mpaka sasa chama kimekwisha mlipa Tshs. 175,000,000/=Baada ya kupata wadhifa wa Makamu Mwenyekiti, na kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha Wilayani na Makao Makuu niliamua kumshauri MBOWE asitishe kujilipa deni kutokana na fedha za ruzuku kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopita kunaendana na utaratibu wa usimamizi wa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa toka serikalini.
Saturday, 18 January 2014
Freeman Mbowe : Kupewa pesa na Kikwete au CCM si tatizo

“Mimi ni mbunge, bungeni nimekuwa nikichangia watu mbalimbali mimi kama Freeman, si ajabu watu wengine kunichangia. Hapa jambo la msingi ni kwamba unapewa pesa kwa sababu gani, kwa nia ipi? Kupewa pesa na Kikwete au CCM si tatizo lakini unapewa pesa kwa sababu zipi, kwa malengo gani?” alihoji Mbowe.
Mbunge Temeke akabidhi madawati 500 shule za msingi

CCM Zanzibar wajipanga kukwamisha Serikali tatu

Wabunge na Wawakilishi wa CCM Zanzibar tayari wamekutana na kupanga mkakati wa pamoja kwa nia ya kupinga Mfumo wa Muungano wa Serikali tatu uliopendekezwa katika Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imefahamika juzi visiwani Zanzibar. Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa kikao hicho kilifanyika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwanduwi kuanzia saa 9.00 Alasiri hadi saa 1:00 ya usiku chini ya Uenyekiti wa Makamo wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vua.
Vyuo vikuu wampendekeza January Makamba kuwa Rais ajaye
Mmoja wa Mashabiki wa January Makamba, akibusu picha ya Mbunge huyo aliyoitumia wakati wa kampeni za Ubunge mwaka 2010.
UMOJA wa viongozi wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania umempendekeza Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba, kuwa ndio anayefaa kuwania nafasi ya Urais katika uchaguzi ujao wa mwaka 2015 kwakuwa hajawai kuhusishwa na kashfa za rushwa na ufisadi . Umoja huo unakusudia kutembea nchi nzima kwajili ya kushawishi wananchi kumchagua Makamba katika kinyanganyiro cha na nafasi ya urais katika uchaguzi ujao kwakuwa ndio kiongozi atakayeleta matumaini mapya.
NCCR kuwa chama kikuu cha upinzani baada ya uchaguzi 2015
Ndugu zanguni,
Kama mjuavyo kwa sasa kinaendelea kunuka ndani ya chadema, chama ambacho ni kikuu cha upinzani nchini. Jambo hili la timua timua na kuumbuana wazi wazi kwa viongozi wa ngazi ya juu chadema imekifanya chama hiki kipoteze mvuto na heshima mbele ya jamii. Wakati huo huo, Chama kizoefu na chenye wasomi waliobobea , NCCR mageuzi wamekuwa kimya huku wakijiimarisha zaidi na kujijengea heshima kubwa m,bele ya jamii kwa kufanya harakati zao bila vurugu na bila kuwa kwaza watu
Mwigulu Aimega CUF,Avuna Wanachama Wapya 146,Afungua Mashina Ya CCM Tandahimba

Naibu Katibu Mkuu akizindua Shina la Wakereketwa Kata ya Chitama wilaya ya Tandahimba hii jana Tar.18/01/2014,Hapa akipandisha Bendera ya Chama iendelee Kupepea kama na Kuwaangaza wote wanaoamini katika Umoja na Amani ya Nchi yetu
Zengwe la kumkwamisha Lowassa kugombea urais hili hapa

MKAKATI wa Edward Lowassa kutaka kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huenda ukakwama baada ya baadhi ya vigogo ndani ya chama hicho kupanga mkakati wa kutaka kumfukuza, imefahamika. Taarifa za ndani ya CCM zinasema mpango wa kutaka kumfukuza Lowassa kutoka chama chake unatokana na hofu ya baadhi ya wagombea wenzake wanaohaha kutaka kumrithi Rais Jakaya Kikwete mwaka 2015.
RIPOTI YA UCHUNGUZI BINAFSI JUU YA MGOGORO NDANI YA CHADEMA
RIPOTI YA UCHUNGUZI BINAFSI JUU YA MGOGORO NDANI YA CHADEMA
Mimi ni Raia wa Tanzania, sina uanachama wa chama chochote cha siasa na sina ushabiki na kiongozi yeyote wa kisiasa. Nitawasilisha uchunguzi wangu binafsi juu ya mgogoro unaoendelea hivi sasa ndani ya chadema
Nitaanza kwa kuzungumzia kile ambacho nimekuwa nikikiona hasa kwenye mitandao na hata stori za vijiweni.
- Tuhuma namba moja ni tuhuma dhidi ya Zitto kwamba amenunuliwa na CCM ili kukiharibu chama
- Tuhuma namba mbili ni tuhuma kwamba Zito anaonewa na viongozi wa juu, Slaa na Mbowe (hapa pia ukabila umeingizwa na udini pia)
Friday, 17 January 2014
FREEMAN AIKAELI MBOWE AMEZAA WATOTO 2 NA JOYCE MUKYA

Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe akiingia katika ofisi za mkoa za Jeshi la Polisi mkoni Arusha ,aliyevaa nguo nyeusi ni Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema,Joyce Mukya akiwa amemsindikiza mwenyekiti wao Polisi.
Kumbe Mwenyekiti wa Chadema , Freeman Aikaeli Mbowe , Amezaa watoto 2 na mbunge wa viti maalumu chadema , Joyce Mukya .
Hii imedhibitika kwenye msiba wa dadake mbowe ambapo joyce mukya alienda na watoto hao kitu kilichosababisha lilian mbowe kukimbia msiba baada ya mbowe kugoma kumfukuza mukya katika msiba huo . Lilian mbowe alikimbilia kwao tengeru kwa babake .
Na MABADILIKO CHADEMA
Subscribe to:
Comments (Atom)


